Watu 12 Hufa na Waniger 27,000 Huachwa Bila Makazi Kutokana na Mafuriko

Flooding in Niamey in Niger - Public Domain

Mafuriko mjini Niamey, nchini Niger – Miliki ya Umma

Mvua kubwa na mafuriko nchini Niger yamewaua watu 12 na kuacha maelfu bila makazi. Mito katika Niamey na maeneo ya karibu imefurika na kuharibu maelfu ya nyumba. Katika kanda, uharibifu wa ardhi na kilimo pembezoni mwa ardhi huzidisha hatari ya kwamba matukio yaliyokithiri yanaweza kubadilika kuwa maafa ya asili. Baadhi ya masuluhisho ya kujiandaa dhidi ya mafuriko yalikuwa yanatekelezwa na mamlaka za kitaifa:

ANADIA Niger ina malengo ya kuendeleza mbinu na zana za kutathmini hatari ya mafuriko, kutegemeza mipango kwenye viwango tofauti vya uamuzi, kuzidisha ujasiri wa jamii, na kuendeleza uwezo mkubwa zaidi wa kutabiri na kuitikia. Kwenye muktadha huu, uundaji wa hifadhidata ya mafuriko utachangia katika uamuzi wenye ufanisi mkubwa zaidi.

 

1 maoni

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.