Honduras Yazalisha Ajira kwa Kuhamasisha Shughuli za Jamii

Rais wa Honduras Juan Orlando Hernandes amezindua mpango wa “Desarrollemos Honduras” (Tuiendeleze Honduras), na maofisa na jamii walishiriki katika tukio hilo. Hernandes alieleza kwamba kama nyumba imebomoka au sakafu yake ni ya udongo, matengenezo lazima yafanyike kwa kutumia sementi; au kuweka vipaumbele kulingana na mahitaji ya familia, na:

Cambiar los fogones tradicionales por los ecofogones. Yo sé que en muchos lugares, tal vez no sea el caso de las casas aquí, es triste preguntarle a la gente cuánto paga por la leña y la gente no sabe, hay que explicarle (…) A veces a la gente se sale más cara la leña que la comida.

Kununua majiko ya kisasa badala ya mafiga za kizamani. Ninajua kwamba kwenye maeneo mengi, huenda sio hapa, inahuzunisha kuuliza kiasi gani cha pesa watu hutumia kununua kuni na hawajui, sisi ndio twapaswa kuwaeleza (…). Mara nyingine, watu hulipa fedha nyingi kununua kuni kuliko wanavyogharamia chakula.

Watumiaji wa mtandao wa Twita waliweka picha na maoni yao:

TUIENDELEZE HONDURAS ilianza leo kwenye jamii ya El Reparto. Mpango huo wa kuendeleza majirani utatengeneza nafasi 150 za vijana wanaotoka kwenye jamii hizo.

Hii kwa kweli inafaa, sote tushirikiane ili mambo yawe bora zaidi. Tuiendeleze Honduras.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.