Namna ya Kuwa Baba Mwema

padreehijo

Picha ya Lon Queta kwenye mtandao flickr (CC BY-NC-SA 2.0).

Raia wa Panama Joel Silva Díaz anafafanua kile ambacho kinawashangaza watu wengi, hususani wanaume: namna ya kuwa baba mwema. Kwenye blogu yake anaeleza changamoto alizokutana nazo na baba yake mwenyewe na kuhusianisha na malengo yake kama baba:

…Recuerdo que veía como un juego el buscar un tema de conversación, debido a mi falta de interés en el deporte, nunca tuvimos una conversación de más de 5 líneas (legítimamente contadas por más de 10 años), pero conociendo otros casos e historias, por lo menos tuve un padre.
[…]
Y es eso lo que quiero mejorar, quiero ser un padre que no haga las cosas sin enterarse, quiero abrazar, quiero besar a mis hijos, presentarle siempre la opción de tomar las mejores decisiones y apoyarlos cuando no tomen las mejores, nunca dudar en mostrarles mi amor y cariño, mucho menos dudar cuando se ganen un coscorrón.
[…]
Pero mi parte no quiero que se quede en un apellido, o un cheque en la quincena, mi parte ha de ser presente, determinante y quiero que mi hijo o hija tenga por lo menos un solo recuerdo lindo impregnado en su corazón, como los domingos de Salsa y el olor a grama recién cortada de los domingos en mi casa.

Nakumbuka mchezo wa kuangalia cha kusema, shauri ya kutokupenda kwangu michezo hatukuwahi kuwa na mazungumzo ya zaidi ya mistari mitano (kwa uhakika kabisa nakumbuka kwa zaidi ya miaka kumi), lakini kwa kufahamu mahusiano yetu katika maeneo mengine, angalau naweza kusema nilikuwa na baba.
[…]
Na hicho ndicho ninachotaka kukifanya vizuri zaidi, nataka kuwa baba anayefanya bila hata kutambua, nataka kuwakumbatia, kuwabusu, kuwapa fursa bora za kufanya maamuzi bora na kuwasaidia wanapokuwa hawajafanya chema, sichelewi kuwonyesha upendo na kuwajali, hata kama kuna nyakati naweza kweli kuwafinya.
[…]
Kwangu, nisingependa jina la mwisho liishie, wala kuwachungulia kila baada ya majuma mawili, napaswa kuwepo, kuamua, na ninataka watoto wangu wawe na angalau kumbukumbu moja nzuri akilini mwao, kama mwanangu Salsa anavyokumbuka harufu nzuri ya majani yanapokuwa yamekatwa siku za Jumapili nyumbani.

Je, wewe ni, au unapanga kuwa baba mwema?

Unaweza kusoma zaidi anayoyaandika Silva Diaz kwa kumfuatilia kwenye akaunti yake ya G+ au Twita

Makala haya ni sehu ya kumi na moja ya #LunesDeBlogsGV, (Jumatatu ya blogu kwenye GV) siku ya Julai 14, 2014.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.