Mjadala Kuhusu Upatikanaji wa Mtandao wa Intaneti Wazidi Kushika Kasi Nchini Cuba

Foto Sandra Abd'Allah-Alvarez Ramírez

Picha na Sandra Abd'Allah-Alvarez Ramírez

Bila shaka yoyote, suala la mawasiliano nchini Cuba ni miongoni mwa mada inayofuatiliwa kwa ukaribu kabisa wakati huu. Kutokuwepo kwa namna rahisi na ya haraka ya kupata mawasiliano limekuwa si jambo linalozungumzwa sana katika kisiwa hiki, lakini pia mijadala imeshika kasi popote pale waishipo watu wa Cuba, na hii ni kutokana na umuhimu wa njia hii ya mawasiliano baina ya ndugu na marafiki.

Makala mbalimbali kuhusiana na tatizo la mtandao wa intaneti nchini Cuba zinasambaa katika mitandao mbalimbali nchini humo. Zifuatazo ni makala tatu miongoni mwa makala nyingi zinazosambazwa.:

ETECSA yatoa ufafanuzi

Alhamisi iliyopita, tarehe 16 Juni, maafisa kutoka kampuni ya mawasiliano ya Cuba(Empresa de Telecomunicaciones de Cuba, ETECSA), kampuni pekee nchini humo, iliweza kushiriki katika Jukwaa la mtandaoni lililoandaliwa na jarida la Cubasi.cu.

Wakati wa uwasilishaji mada, ETECSA iliweka bayana kuwa:

El posicionamiento de nuestros servicios es frecuentemente comparado con la asequibilidad y facilidades que ofertan los operadores de telecomunicaciones de otros países, incluidos los de la región de Latinoamérica. En la medida que se desplieguen las inversiones necesarias, nuestra empresa podrá lograr índices cada vez más comparables en cuanto a calidad y desarrollo,  y ampliará la infraestructura de telecomunicaciones, posibilitando la disminución de los precios y asimilando un mayor ritmo de crecimiento y diversificación de los servicios. 

Hali ya huduma ya mawasiliano katika nchi yetu mara nyingi imekuwa ikilinganishwa na urahisi wa upatikanaji na utoaji wa huduma hizi kutoka kwa wamiliki wa njia za mawasiliano kutoka nchi nyingine, ikiwa ni pamoja na maeneo ya Amerika ya Kusini. Wakati ambapo uwekezaji muhimu unapoanza kuonekana, kampuni yetu itafikia kiwango cha ushindani kwa kuzingatia ubora na ubunifu, na hivyo miundombinu ya mawasiliano itaongezeka, hali itakayopelekea kupungua kwa gharama na kuwezesha kukua kwa haraka njia za mawasilino na utoaji wa huduma nzuri.

katika mijadala ya mtandaoni maswali yalijikita zaidi kwenye huduma za kitaifa za simu za mikononi, gharama na na upatikanaji wa huduma ya intaneti, wakizungumzia hali ya kutokuwapo kwa uwezekano wa kupata huduma ya intaneti watu wakiwa majumbani mwao. Katika mtazamo huu, Yosiel, aliuliza;

¿Por qué no es posible aún poner Internet en los domicilios a cubanos residentes en Cuba a precios asequibles?, y no me refiero a la infraestructura del típico desastre del Módem a 56 Kb con la inversión que esto necesita que además sabemos no es de buena calidad, me refiero a por qué no poner en cada central telefónica un buen o 4 buenos equipos de red inalámbrica y así cualquiera accedería desde su casa con su Smartphone, PC, Laptop, etc. A la red de redes a velocidades parecidas en salas de navegación de ETECSA misma.

Kwa nini hadi sasa huduma ya intaneti haijawezekana kupatikana kwenye makazi ya watu wa Cuba kwa gharama nafuu? Na hapa sizungumzii modem, kifaa hafifu kilicho na uwezo wa KB 56 na aina ya uwekezaji unaopaswa kuzingatiwa, ikizingatiwa pia na uzoefu tulionao, huduma hii haipo katika kiwango kinachotakiwa. Ninachokimaanisha hapa ni kuwa, ni kwa nini wasiweke chanzo kimoja au vinne vya mtandao wa intaneti wa si-waya ili kila mmoja aweze kupata huduma ya intaneti akiwa nyumbani kwake kupitia simu yake, ngamizi ya kawaida, ngamizi mpakato n.k ikiwa na kasi ifananayo na ile inayopatikana katika vituo vya ETECSA.

ETECSA responded:

La estrategia de ETECSA prevé el acceso a estos servicios desde los hogares; pero la prioridad inicial de la empresa ha sido ampliar las salas de navegación colectivas, para garantizar el acceso a un mayor número de personas.
En estos momentos, no resulta posible la generalización inmediata del acceso a Internet, dadas las limitaciones técnicas. No obstante, ETECSA se encuentra ejecutando inversiones que posibiliten la implementación de estos servicios con las condiciones técnicas requeridas y a precios inferiores a los actuales.

Mkakati wa ETECSA ni kuwa, siku zijazo mtandao upatikane hadi majumbani, hata hivyo, mpango wa awali wa kampuni ni kuongeza matawi yake ili watu wengi zaidi waweze kupata huduma.
Katika kipindi hiki, na kwa kuzingatia vikwazo vya kiufundi, haiwezekani kwa haraka kuwezesha watu kupata huduma ya intaneti wakiwa majumbani mwao. Hata hivyo, , ETECSA inaangalia namna ya utoaji wa huduma utakaochochea utoaji wa huduma kwa kuzingatia uwezo wa kiufundi na kwa gharama za chini zaidi ikilinganishwa na hali ilivyo sasa.

Tovuti zilizozuiwa: Zipitie leo, na labda sio kesho

Mnamo Juni 19, raia kadhaa pamoja na vyombo vya habari vilithibitisha kuwa, tovuti zilizokuwa zimezuiwa, zilianza tena kutumiwa kisiwani humo, miongoni mwa tovuti hizo maarufu, moja wapo ikiwa ni Skype. 

Majukwaa mengine ya kidigitali kama vile jarida la 14ymedio.com linalosimamiwa na mwanablogu Yoani Sánchez, ambalo kabla ya kurudishwa tena rasmi, lilielekezwa yoanilandia.com, hali iliyopelekea kushindikana kwa jarida hili kutembelewa na watu wakiwa kisiwani humu (hali iliyopingwa vikali) limekuwa tena likipatikana kupitia mtandao wa intaneti nchini Cuba. Revolico.com, jukwaa la biashara ya kupitia elekroniki la Cuba linaloshabihiana na craigslist, pia lilianza kupatika mtandaoni kwa watembeleaji waishio Cuba. Hata hivyo, mnamo Juni, 20, baadhi ya watumiaji wa mtandao wa Facebook walipelekewa ujumbe kuwa, tovuti hizi zimeshazuiwa tena. Nchini Cuba, msemo maarufu unasema kuwa, “Furaha katika nyumba ya mlala hoi haidumu”  

Uhuru wa upatikanaji wa huduma ya intaneti

Kimantiki,gharama za upatikanaji wa mtandao wa intaneti kwa watu wa Cuba zinaelezewa na Mhandisi wa masuala ya mawasiliano, Norges Rodriguez, ambaye pia ni mmiliki wa blogu ya  Salir a la manigua, anatembeza hati ya makubaliano ya mtandaoni katika Change.org, yanayoilenga mamlaka ya Cuba, hususani Waziri wa Mawasiliano, Maimir Mesa Ramos.

Miongoni mwa sababu za ombi hili ni:

Por  la trascendencia de las nuevas prácticas sociales que ofrece Internet que puede ser comparada solo con las que ofrecieron en su momento la aparición de la escritura, la imprenta, la radio, la telefonía, la televisión, y negarla sería negar el desarrollo.

Mambo mapya yanayofanyika hivi sasa miongoni mwa wanajamii yaliyowezeshwa kwa uwepo wa mtandao wa intaneti ni mambo ya kuzingatia na yale tu yawezayo kulinganishwa na yale yaliyokuwa yanatolewa kwa wakati wao. Utendaji Mpya wa kijamii uliowezeshwa na mtandao wa intaneti ni msingi na unaweza kufananishwa na ule unaoletwa, kwa wakati wake, yaweza kuwa uharaka wa uandikaji, uandishi wa habari, redio, huduma za simu, kuzuia mambo haya ni sawa na kuzuia maendeleo.

Katika suala hili, jambo hili linaonekana kuwa ni geni pale ambapo mwanablogu kutoka katika kisiwa hiki kuanzisha kampeni za mtandaoni. Siku za nyuma, kampeni ya mtandaoni iliyokuwa na lengo kama hili ilipewa nafasi kubwa Nchini Cuba, tunahitaji gharama muafaka za upatikanaji wa mtandao wa intaneti katika simu za mkononi lakini ni kutoka Florida, Marekani, katika wavutiCubanet

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.