Mradi Wa Kutumia Simu za Mkononi Kuhamasisha Usomaji

Lauri anaandika kuhusu mradi uliopo Afrika Kusini, Mfuko wa Usomaji wa FunDza, unaotumia teknolojia ya simu za mkononi kuhamasisha tabia ya kusoma kwa watoto:

Kinachofurahisha, hata hivyo, ni pale Waafrika wanapopata majibu ya kiubinifu kwa matatizo yao. Mradi wa FunDza ni mfano moja wapo. Simu za mkononi zimeenea sana nchini Afrika Kusini na FunDza wanalenga kuwasaidia watoto wapende kusoma. Ninajisikia fahari kuandika mara kwa mara kwa ajili yao.

Namna inavyofanya kazi ni kwamba hadithi inaanza Ijumaa. Kila hadithi ina sura saba na sura moja inatumwa kwenda kwennda kwenye simu za watoto kila siku. Hapa ni ukurasa wa mwandishi wenye hadithi zote nilizoandika kwenye mradi wa FUnDza. Bofy kwenye hadithi yangu kuona maoni yanayoanhwa na wasomaji. Watoto wanasoma na kuhusika na hadithi! Ninadhani hatua hii ni kubwa!

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.