Madagaska Bado Inasubiri Waziri Mkuu, Serikali Mpya

Mwezi mzima tangu Rais mteule  Hery Rajaonarimampianina achaguliwe kuwa mkuu wa nchi nchini Madagaska, bado hakuna dalili nani atakuwa waziri mkuu na akina nani wataunda serikali. Ma-Laza anahoji kuwa suala kuu si hasa nani atakuwa waziri mkuu bali atakuwa ana ajenda gani akikabidhiwa ofisi [fr]: 

 Un  technicien hors pair,  rassembleur, capable de mener à bien la politique générale du Président de la République. Ce Premier ministre ne  devrait appartenir à aucune mouvance politique, en principe.Mais il n’est ni contre Rajoelina, ni contre Ravalomanana. Bref, c’est un oiseau rare qui inspire aux bailleurs de fonds la confiance. Cette personne existe-t-elle ?  

(waziri mkuu lazima awe) mtu mwenye wasifu wa weledi, mtu atakayewaunganisha watu na mwenye uwezo wa kushughulikia sera za Rais wa Jamhuri. Kinadharia, Waziri Mkuu lazima asiwe sehemu ya harakati za siasa. Hatakuwa kinyume na Rajoelina, wala  Ravalomanana (marais wawili waliopita). Kwa kifupi, lazima awe mtu nadra atakayewafanya wawekezaji wavutiwe kuja. Swali ni:  hivi mtu wa namna hii yupo kweli?

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.