Shirika la UNICEF Latoa Wito wa Kutokuweko kwa Watoto Katika Maandamano Nchini Thailand

Baada ya mlipuko wa bomu la kurushwa kwa mkono nakuwauwa watoto watatu katika maandamano ya kupambana na serikali katika eneo la Bangkok, Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa lilitoa wito kwa serikali na viongozi wa maandamano kuwalinda watoto na kuwaweka mbali na maandamano. Bijaya Rajbhandari, Mwakilishi wa UNICEF nchini Thailand, ametoa wito huu:

(UNICEF) inalaani vurugu ambayo ilisababisha maafa haya na vifo vya kipumbavu na majeraha kwa watoto. Matukio haya kusisitiza haja ya haraka ya kuweka watoto nje ya njia ya madhara ili kuhakikisha usalama wao. UNICEF inataka Serikali, na viongozi wa maandamano dhidi ya serikali na wazazi wote kuhakikisha kuwa watoto hawaingii katika maeneo ya maandamano na kutunzwa vizuri mbali na maeneo yote ya maandamano..

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.