Sababu 10 Kwa nini Siafiki Shariah Nchini Pakistan

Mmoja wa msemaji wa Taliban alijitoa kwenye majadiliano ya hivi karibuni na serikali ya Pakistan na kudai kuwa ajenda ni pamoja na kuanzishwa kwa sharia kali. Mwanablogu wa Pakistan na Mwandishi wa Habari Beena Sarwar alipinga wazo hilo kupitia tamko aliloliweka katika mtandao wa Facebook lenye kichwa cha habari ‘sababu 10 kwa nini sitaki Shariah nchini Pakistan’ na linapatikana katika mitandao mingine ya kijamii kamaKusitisha Udini Pakistan, harakati za kupinga ukandamizaji, ubaguzi, kuvuka mipaka na uvumilivu na Uchaguzi wa Pakistani linaloendeshwa na Asasi za Kiraia. Hapa ni baadhi ya sababu:

1. Dini na ninavyochagua kuishi ni biashara yangu na ni suala lisiloihusu Serikali.

2. Kutekeleza Shariah hakutanifanya kuwa muislamu bora wala kuboresha hali ya mambo nchini Pakistan. Mataifa yote yaliyoendelea yanatawaliwa na serikali zisizo za kidini.

3. Kukataa wazo kwamba Shariah kwa namna yoyote inaweza kutekelezwa na wale ambao wamebaka na kupora nchi yangu, kulipua shule na misikiti na kukata askari vichwa. Sitawapa wahalifu hawa haki ya kuniamrisha.

4. Sitasalimisha haki yangu ya kiraia, ikiwa ni pamoja na uhuru wa mawazo na kujieleza, chini ya kivuli cha Shariah..

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.