India: Saa Nzuri Kapata Huduma za Afya Hospitalini kwa Punguzo la Bei

Kamayani wa mtandao wa Kracktivist anasema kuwa dhana ya saa nzuri kupata punguzp la bei, ambayo ni maarufu sana kwenye vilabu vya pombe, mahotelini na hata kwenye majengo ya sinema, imeingia hadi kwenye sekta ya afya nchini India. Hospitali binafsi iliyoko Bangalore siku za hivi karibuni imekuwa ikitoa punguzo la bei kati ya asilimia 30-75 kwa huduma muhimu, ikiwa ni pamoja na uchunguzi, kufanyiwa vipimo vya x-ray na hata ushauri, wakati wa masaa yasiyo yasiyo na shughuli nyingi. Hosptali nyingine zinajiandaa kufuata mkondo huo hivi karibuni.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.