Madaktari 400 wa Cuba Waenda Brazil

Daudi Oliveira de Souza, daktari na profesa wa Taasisi ya Utafiti wa Hospitali ya Sirio-Libanés, alituma barua ya wazi kwa madaktari zaidi ya mia nne wa Cuba ambao hivi karibuni waliwasili nchini Brazil wanaoanzisha kundi la kwanza la jumla ya madaktari 400 ambao wanatarajiwa kuja nchi hii kabla ya Desemba mwaka huu.

Maternal home in Cuba. (Foto: Randy Rodríguez Pagés)

Nyumba ya Wajawazito nchini Cuba. (Picha: Kurasa za Randy Rodríguez)

Chapisho la Missive, linalochapishwa na Folha kila siku kutoka Sao Paulo, linasema:

Karibu, madaktari wa Cuba. Mtakuwa muhimu sana kwa ajili ya Brazil. Ukosefu wa madaktari katika maeneo ya mbali kijijini umewafanya watu wetu kuwa katika hali ngumu. Msijali kuhusu uadui kutoka kwa baadhi ya wafanyakazi wetu. Mtapata fidia sana kwa makaribisho mazuri katika jamii ambazo mtatoa huduma kuanzia sasa.

Kwa mujibu wa Oliveira de Souza, katika majimbo kama Sergipe, ni rahisi kuhama kutoka mji mkuu hadi miji ya Ndani, lakini hata hivyo kuna mamia, ya nafasi za kazi zisizotumika hata katika vitengo vya afya vyenye vifaa na vilivyoko katika hali nzuri.

Kabla ya upungufu wa madaktari 14,500 katika taifa la Amerika ya Kusini, serikali ya Dilma Rousseff ilipitisha sera ya “Mais Medicos” (mpango wa Madaktari Zaidi), ambayo itaweka mikataba na madaktari kutoka Hispania, Ureno, na Cuba, kati ya mataifa mengine.

Hivi karibuni, mmojawapo wa wakosoaji wakubwa wa makubaliano hayo na wa-Cuba anasema kwamba “walikuwa wanatumiwa bila faida.” Kwa hoja hii, Oliveira de Souza anasema:

Ni mapema mno kuongelea kama wao watafanya kazi kama watumwa. Panamerican Health Organization (PHO), yenye karne ya uzoefu, watakuwa washirika wazuri, tangu kutiwa saini kwa mkataba wa ushirikiano na serikali ya Brazil. Nyuso zao za furaha katika viwanja vya ndege zilionyesha matumaini. Kwa lugha ya kijijini kwetu, kufuatia idadi kubwa ya madaktari wetu, naweza kusema tu kwa imani: nawakumbatia kindugu na asante sana.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.