Peru: Wafanyabiashara Wachoma Nguo Kupinga Bidhaa za Kichina

Wafanyabiashara kutoka eneo la Gamarra [es], kituo maarufu cha viwanda vya nguo na ambako ndiko lilipo eneo la kibiashara jijini Lima, walichoma nguo zilizoingizwa kutoka China [es] katika mitaa kupinga biashara hiyo ya nguo zinazouzwa bei ndogo ambazo, kwa mujibu wao, hufanya biashara zao kufilisika.

Kwenye mtandao wa Twita, Alfredo “Alial” (@ Alfredo_jch) [es] alipendekeza matumizi bora kwa nguo hizo zilizoteketezwa kwa moto:

Jijini Gamarra wanachoma moto nguo za Kichina, huko Puno watu wanaganda hadi kufa [kwa kukosa nguo]. #Perú

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Jimbo la Carabaya, lililoko katika mkoa wa Puno, lilishuhudia dhoruba kali ya theluji mbaya zaidi kuwahi kutoka katika kipindi cha muongo, ikiathiri familia zaidi ya 1,200 na kuwaacha watu wengi wasiojulikana walipo na kusababisha vifo vya wanyama ambao ni riziki ya watu wa eneo hilo.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.