Wafanyabiashara kutoka eneo la Gamarra [es], kituo maarufu cha viwanda vya nguo na ambako ndiko lilipo eneo la kibiashara jijini Lima, walichoma nguo zilizoingizwa kutoka China [es] katika mitaa kupinga biashara hiyo ya nguo zinazouzwa bei ndogo ambazo, kwa mujibu wao, hufanya biashara zao kufilisika.
Kwenye mtandao wa Twita, Alfredo “Alial” (@ Alfredo_jch) [es] alipendekeza matumizi bora kwa nguo hizo zilizoteketezwa kwa moto:
En Gamarra queman la ropa China, en Puno la gente muere de frío. #Perú
— Alfredo ”Alial” (@Alfredo_jch) August 28, 2013
Jijini Gamarra wanachoma moto nguo za Kichina, huko Puno watu wanaganda hadi kufa [kwa kukosa nguo]. #Perú
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Jimbo la Carabaya, lililoko katika mkoa wa Puno, lilishuhudia dhoruba kali ya theluji mbaya zaidi kuwahi kutoka katika kipindi cha muongo, ikiathiri familia zaidi ya 1,200 na kuwaacha watu wengi wasiojulikana walipo na kusababisha vifo vya wanyama ambao ni riziki ya watu wa eneo hilo.