Shambulio la Kigaidi Laua Watu Watano Mjini Bamako

Screen capture of police forces in Bamako, Mali after the terrorist attack

Picha ya majeshi ya polisi mjini Bamako, Mali baada ya shambulio la kigaidi

Shambuliko la kigaidi lilitekelezwa kwenye mgahawa jijini Bamako, makao makuu ya Mali, limechukua maisha ya watu watano usiku wa siku ya Ijumaa mnamo Machi, 6. Shambulio hilo lilifanyika usiku wa maneno kwenye mkahawa unaoitwa took Terrasse kwenye mitaa ya Bamako na watu zaidi ya kumi wamejeruhiwa vibaya. Washukuiwa wawili wamekamatwa na wanaendelea kuhojiwa na vyombo vya ulinzi na usalama. Afisa wa polisi aliripoti kwamba watu   hao wawili walikuwa na silaha kali pamoja na mavazi ya kijeshi. Mtu mmoja alilipua bomu kwenye mkahawa. Raia wawili wa watatu, Mfaransa mmoja na raia mwingine wa Ubelgiji waliuawa. Mwanablogu mmoja aliweka video inayoonesha vikosi vya polisi waliokuwa wakifanya uchunguzi kwenye eneo la tukio:

Mchangiaji wa Global Voices Marc- André Boisvert aliandika kwenye mtandao wa twita kwamba shambulio kama hilo halikuwa linaepukika, kwa sababu Mali bado inajitahidi kurudisha hali ya amani kwenye ukanda huo wa Kaskazini:

Sote tulijua tukio hili lingetokea mjini Bamako. Sote tunajua shabaha ilikuwa kuwalenga wapiga kelele. Lakini bado tunashangazwa

Philippe Paoletta, mkazi wa Bamako, anakubaliana na Marc-André:

Kila moja alijua yaliyotokea yangetokea wakati fulani hapa Bamako. Hata hivyo hiyo haifanyi hali hiyo isiwe ya kushangaza. Mwenyezi Mungu aziweke pema roho za marehemu

 

Tunawatakia majeruhi wa shambulio kupona kwa haraka.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.