2015 Mwaka wa Kufanyika Chaguzi Huru na Haki Barani Afrika

Wekesa Sylvanus anataraji kwamba 2015 utakuwa mwaka wa chaguzi huru na haki barani Afrika:
https://wekesasylvanus.wordpress.com/2015/02/18/will-2015-be-a-year-of-free-and-fair-elections-in-africa/

Tangu kurejeshwa kwa mfumo wa demokrasia ya vyama vingi barani Afrika, ushindani nyakati za uchaguzi umekuwa suala la kufa na kupona kwenye nchi nyingi za ki-Afrika. Chaguzi barani Afrika ni suala lenye hatari zake na katika nyakati za hivi karibuni, chaguzi zimekuwa kichocheo cha migogoro. Kenya na Ivory Coast ni mifano mizuri ya namna kutokusekana kwa utaratibu mzuri wa uchaguzi kunavyoweza kuiingiza nchi kwenye machafuko. Karibu nusu karne baada ya uhuru, nchi nyingi za ki-Afrika hazijaweza kuwa na taratibu sahihi kufanya chaguzi zilizo huru na haki. Mwaka 2015 utashuhudia nchi nyingi zikiingia kwenye uchaguzi. Chaguzi za Rais na/au wabunge zitafanyika kwenye nchi za Naijeria, Sudan, Ethiopia, Burundi, Tanzania, Zambia, Togo, Ivory Coast, Mauritius, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Burkina Faso, Naija, Guinea, Chadi, na Misri na labda Sudani Kusini kutegemeana na makubaliano ya amani yanayotarajiwa kuwekewa saini. Nyingi za nchi hizi zimepambana kutaasisisha utendaji wa kidemokrasia katka siku za hivi karibuni. Mwaka 2015 unaleta fursa kubwa kwa nchi hizi kuionesha dunia kwamba sasa zimekomaa kidemokrasia.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.