Kolombia: Hapana kwa Utalii wa Ngono Mjini Medellín

NoTurismoSexual

“Hapana kwa utalii wa ngono “. Picha mnato ya video iliyowekwa kwenye mtandao wa YouTube.

Kufikia katikati mwa mwezi Julai 2014, ukurasa wa Facebook Hapana kwa utalii wa ngono ulianzishwa, kwa lengo la kukuza uelewa kuhusu utalii wa ngono nchini Kolombia. Wikipedia inatafsiri dhana hiyo:

… una forma de turismo con el propósito de mantener relaciones sexuales, normalmente de varones con prostitutas hembras, pero también, aunque menos, hay mujeres turistas sexuales y turismo sexual homosexual masculino.

Utalii wa ngono ni safari zinazohusisha vitendo vya gono, hususani na kahaba. Shirika la Utalii Duniani , chombo maalum cha Umoja wa Mataifa, unatafsiri utalii wa ngono kama “safari zinazofanywa ndani ya sekta ya utalii au nje ya sekta hii lakini kwa kutumia muundo na mtandao wake, kwa lengo kuu la kuathiri kwa namna moja au nyingine uhusiano wa ngono za kibiashara kati ya mtalii na mkazi wa eneo analokwenda kulizuru “.

Hivi karibuni, ukurasa huo wa Facebook uliweka video hii, kama sehemu ya kampeni iliyowekwa na Mfuko wa Pazamanos kwa lengo la kuwakataa watalii wa ngono ambao mara nyingi hutembelea jiji la Medellín.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.