Jinsi Wanablogu Walifikia Gerezani kwa Kuandika Kuhusu Haki za Binadamu Nchini Ethiopia

Melody Sundberg anachambua uhuru wa kujieleza nchini Ethiopia baada ya wanablogu wa Ethiopia waliokamatwa kukaa siku 100 gerezani:

Ethiopia ina idadi ya watu 94,000,000 na ni nchi ya pili yenye wakazi wengi katika bara la Afrika. Hata hivyo, hailingani na mahojiano ya Endalkhachew Chala kupitia Global Voices, kuwa na gazeti huru la kila siku au vyombo vya habari huru. Kulikuwa na haja ya sauti mbadala na kwa hivyo Zone 9:ers walianza kublogu na kutumia vyombo vya habari vya kijamii kwa kuandika juu ya mada zinazohusiana na haki za binadamu. Jina la kundi, Zone 9, inawashiria maeneo ya sifa mbaya za gereza la Ethiopia Kality, ambapo wafungwa wa kisiasa na waandishi wa habari wamefungiwa. Gerezani ina maeneo manane, lakini “eneo” la tisa inawashiria Ethiopia. Hata kama ni nje ya kuta za gereza – hauko huru kamwe; mtu yeyote mwenye fikira huru anaweza kukamatwa. Wanablogu walitaka kuwa sauti ya eneo hili la tisa.

Katika mahojiano, Endalkachew anasema kwamba kundi lilikuwa na kampeni kuhusu kuheshimu katiba, kuacha udhibiti na kuheshimu haki ya kuandamana. Kundi pia lilitembelea wafungwa wa kisiasa, kama vile waandishi wa habari Eskinder Nega na Reeyot Alemu. Walitaka kuleta tahadhari kwa umma kwa kutumia vyombo vya habari vya kijamii.

1 maoni

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.