Mfungo wa Ramadhani Wawaingiza Watu Matatani kwa Kula Daku Usiku Nchini Misri

@Shahdan_shosh shares this photograph of 11 young men arrested for having Suhoor - a latenight meal to prepare them to fast the next day during the Muslim month of Ramadan (Source: Twitter)

@Shahdan_shosh aliweka picha hii ya vijana 11 waliotiwa mbaroni kwa kosa la kukutanika kupata daku – chakula kinacholiwa usiku kwa ajili ya kuendelea na fungo wa siku inayofuata wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa Waislamu (Chanzo: Mtandao wa Twita)

Mwaka umepita tangu kung'olewa madarakani kwa rais wa Misri Mohamed Morsi na serikali mpya tayari inakosolewa vikali kwa uvunjifu wa haki za binadamu ikiwa ni pamoja na kukamatwa kiholela kwa raia.

Sheria mpya ya Misri ya kudhibiti mikusanyiko ndiyo hasa imewasha hasira kali miongoni mwa Wamisri, wengi wakijaribu kupinga sheria hiyo lakini hatimaye kujikuta wakikamatwa wao wenyewe, ikiwa ni pamoja na baadhi ya wanaharakati maarufu kama vile Alaa Abd El Fattah, aliyehukumiwa kifungo cha miaka 15 jela mwezi uliopita, kwa ajili ya kuandaa maandamano pasipo kibali.

Kwa siku za kwanza za mwezi wa Ramadhani, mwezi mtukufu wa kufunga kwa Waislamu, vikosi vya polisi vilivamia makazi ya watu na kuwakuta vijana 11 wakipata daku (chakula cha usiku kinacholiwa na Waislamu kabla ya kuendelea na mfungo kwa siku inayofuata), shughuli ambayo inapofanywa na kundi la watu, huonekana kukiuka sheria ya mkutano kama baadhi yao walivyobashiri. Raia mtandaoni walianzisha alama ashiria #معتقلي_السحور [ar], ambayo tafsiri yake ni wafungwa wa daku.

Ahmad Abd Allah aliandika kwenye ukurasa wake wa Facebook yafuatayo [ar]:

١١ واحد بيتسحروا في بيت واحد منهم في دمنهور … الداخلية قبضت عليهم بتهمة التظاهر من غير تصريح … الحرية لمعتقلي السحور

Watu kumi na moja walikuwa wakipata daku usiku katika moja ya nyumba zao. Wizara ya Mambo ya Ndani iliwakamata kwa tuhuma za kufanya mkutano haramu … waachilie huru wafungwa wa daku

Mtumiaji Twita Mohamed Hazem, kutoka Damnhour, alitwi kuwaunga mkono marafiki zake:

Sijui kama mimi nilie kwa sababu ya mauaji yaliyofanywa na walinzi wa serikali au shauri ya rafiki zangu 11 walioko kizuizini

Kwa kejeli baadaye alitwiti:

Je, Wakili wa Serikali atatumia ushahidi wa vyakula vya maharage na mizaituni waliyokutwa nayo?

Na Shahdan-shosh alitwiti picha ya wafungwa hao 11 na kubainisha :

Kosa lao hasa ni hili: Kundi la suhoor. Walikamatwa na (maharage) machafu, falafel na jibini katika nyumba waliyokutwa.

Mwanaharakati Wael Abbas alitwiti kwa wafuasi wake 265000:

Itanibidi pengine mimi kuachana Iftar [chakula maarufu cha swaumu] yangu ya kila mwaka kutii sheria mpya ya maandamano)

Aliongezea:

Hata hivyo, nusu ya wale ambao mimi niliwaalika kwa ajili ya Iftar mwaka jana wako jela, uhamishoni au ni watuhumiwa wa makosa ya jinai)

Mwaka jana, serikali ya Morsi ilijaribu kulazimisha matumizi ya sheria kama hiyo inayozuia mikusanyiko ambayo hata hivyo, haikufaulu baada ya kilio kutoka mashirika ya kimataifa. Blogu ya Misri WikiThawra [ar], ambayo inaendeshwa na Kituo cha Misri cha Uchumi na haki za Kijamii inadai kuwa watu wasiopungua 80 wamefariki wakiwa chini ya ulinzi katika kipindi cha mwaka mmoja na zaidi ya watu 40,000 wamewekwa kizuizini au wako kwenye mashitaka katika kipindi cha mwenzi Julai 2013 (kuiondoa serikali ya Morsi) na katikati ya Mei 2014.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.