Mapigano Dhidi ya Waislamu Yaendelea Nchini Sri Lanka

Yametimu majuma mawili tangu ghasia dhidi ya Waislamu kwenye majiji ya pwani nchini Sri Lank- Aluthgama na Beruwala. Ingawa hali imetulia baada ya kulaaniwa sana kila sehemu, bado ghasia hizo dhidi ya Waislamu zinaendelea katika maeneo tofauti ya Sri Lanka.

Mwanablogu Abdul Khaleq anatwiti kuhusu tukio moja huko Ratmalana sehemu ya wilaya ya Colombo:

Msikiti ulioko barabara ya Ratmalana Borupona umechomwa moto saa 7 usiku. Moto ulioanza mapema ulizimwa.

Mwanablogu D. B. S. Jeyaraj ana habari zaidi kuhusu jaribio lililoshindwa la kushambulia msikiti wa Thalayan Bawa Jumma uliopo kwenye barabara ya Borupane mjini Ratmalana masaa ya asubuhi Jumapili iliyopita, tarehe 29 Juni, 2014.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.