Ousmane Sow : Mwafrika Mweusi wa Kwanza Kushiriki katika Taasisi ya Kifaransa ya Sanaa

Mchonga sanamu Msenegali, Ousmane Sow, alikaribishwa kwenye Académie des Beaux-Arts de Paris [Taasisi ya Sanaa ya Paris] tarehe 11, mwezi wa DisembaAfrica-top-talents.com inaripoti kwamba:

Une belle consécration pour ce sculpteur sénégalais connu pour ses séries de sculptures monumentales consacrées aux ethnies africaines (noubas, peuls, masaï, Zoulou). « Mon élection a d’autant plus de valeur à mes yeux que vous avez toujours eu la sagesse de ne pas instaurer de quota racial, ethnique ou religieux pour être admis parmi vous (…)  Comme mon confrère et compatriote sénégalais Léopold Sédar Senghor, élu à l’Académie française il y a trente ans, je suis africaniste. Dans cet esprit, je dédie cette cérémonie à l’Afrique toute entière, à sa diaspora, et aussi au grand homme qui vient de nous quitter, Nelson Mandela. »

Mchonga sanamu Msenegali, anayejulikana kwa kuchonga mafuatano yake ya sanamu muhimu zinazosawiri kabila za Kiafrika (Wanuba, Wafulani, Wamasai, Wazulu) ametunukiwa tuzo la ajabu. Anasema: “Kuchaguliwa kwangu ni muhimu zaidi kwangu, maanake, kwa hekima yenu [washiriki wa taasisi] hamujawahi kuunda viti maalumu vya kirangi, vya kikabila, wala vya kidini (…) Na kama mwandani wangu na Msenegali mwenzangu, Leopold Sédar Senghor, aliyechaguliwa kuingia Taasisi ya Kifaransa miaka thelathini iliyopita, mimi ni mtaalamu wa mambo ya Kiafrika. Kwa moyo huu, naiweka wakfu hafla hii kwa bara la Afrika, Waafrika wanaoishi nje ya bara hilo, na kiongozi mkuu aliyetuacha hivi juzi, Nelson Mandela.”

1 maoni

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.