Naibu Waziri Ajinyonga baada ya Kushindwa Uchaguzi Nchini Malawi

Blogu ya City Press inaandika kwamba kujinyonga  kwa Godfrey Kamanya,  Naibu Wairi wa Malawi, baada ya kushindwa kukitetea kiti chake cha ubunge kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Mei 20, 2014 :

Matangazo rasmi ya uchaguzi huo uliofanyika Jumanne bado yanaendelea kutangazwa. Lakini matokeo ya awali ya uchaguzi huo yaliyotangazwa na kituo cha redio yalionyesha kuwa Kamanya alikuwa anafanya vibaya kwenye uchaguzi huo na alikuwa na uwezekano mkubwa wa kupoteza kiti chake chake cha ubunge.

Kupitia ujumbe aliouacha ambao kwa sasa upo mikononi mwa polisi, Kamanya anasemekana kusema kuwa aliamua kujinyonga kwa sababu ya migogoro ya kisiasa. Alieleza namna utajiri wake utagawanya na kumwomba Rais aliyeko madarakani Joyce Banda, ambaye alimtumikia, kumsaidia kulipa ada ya shule kwa mwanae.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.