“Hatujaweka Mkazo vya Kutosha Kwenye Afya ya Vijana”

Ripoti ya hivi karibuni kutoka kwa Shirika la Afya Duniani (WHO) kuhusu afya ya vijana duniani inabainisha kwamba

 Sababu kubwa za vifo vya vijana duniani ni ajali za barabarani, VVU?UKIMWI, na kujiua. Duniani kote, wastani wa vijana milioni 1.3 walipoteza maisha yao mwaka 2012.

Ripoti inaongeza vile vile kuwa :

Kiwango cha vifo kimeongezeka miongoni mwa vijana wa umri wa miaka  15  na 19 na pia wale wa umri kati ya miaka 10 na 14. Ingawa baadhi ya sababu za vifo hivyo zinafanana miongoni mwa jinsia, vijana wa kiume wako wanapoteza maisha kwa kasi zaidi kwa sababu ya kujiingiza kwenye vitendo vya matumizi ya nguvu wakati wasichana wakipoteza maisha kwa sababu ya matatizo ya uzazi.    

Baadhi ya sera zinapendekezwa kama hatua nzuri ya kukabiliana na mahitaji ya afya ya akili na ya mwili kwa vijana. Dk. Flavia Bustreo, Mkurugenzi Mkuu Msaidizi wa shirika la Afya ya Familia, Wanawake na Watoto, na Shirika la Afya Duniani   anataja kwamba:

Dunia haijaweka mkazo vya kutosha kwenye afya ya vijana. 

 

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.