Colombia: Watoto 32 Wafariki Kwenye Mkasa wa Moto

Vyombo ya habari Colombia vinaripori [es] vifo vya watoto 32 uliosababishwa na moto katika basi, katika kitongoji cha Fundación mjini Magdalena, Kaskazini mwa Colombia. Tukio hilo la kutisha lilitokea Jumapili mchana, Mei 18, 2014. Hata kama ukweli bado unachunguzwa., Kuna uvumi kwamba gari lilikuwa linasafirisha petroli kimagendo.

Rais wa Colombia Juan Manuel Santos alionyesha huzuni wake kwenye mtandao wa Twita:

Huzuni mkubwa kama baba na kama M-Colombia kwa janga la watoto wetu katika Fundación. Mshikamano, maombi na msaada kwa familia zao.

Twaomboleza kwa ajali katika Fundación, Magdalena, ambapo kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni, angalau watu 15 walifariki, kati yao watoto.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.