Waziri Mkuu wa Zamani wa Malayasia Aitaka Boeing Kuwajibika kwa Ajali ya Ndege MH370

Waziri Mkuu wa zamani wa Malaysia Mahathir Mohamad ameitaka Boeing kuwajibika kufuatia tukio la kupotea kwa ndege ya Shirika la ndege la Malaysia yenye namba MH370. Hivi ndivyo alivyoandika kwenye blogu yake:

Boeing ndiyo imetengeneza ndege hii. Boeing lazima waeleze inakuwaje njia zote za kuifuatilia mwenendo wa ndege hiyo ziweze kuzimwa. Ni ama teknolojia ya Boeing ni duni au haina uhakika. Sitapenda tena kupanda ndege ya Boeing mpaka waeleze kwa nini mifumo yake yote inaweza kuzima kienyeji au kushindwa kufanya kazi.

Boeing lazima wakubali kuwajibika kwa kutengeneza ndege ambayo ingeweza kupotea tu hewani na isionekane tena.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.