Tetemeko Kubwa Lizitikisa Chile na Peru

Sismo

Picha imechukuliwa kutoka kwa mtumiaji wa Twita @24HorasTVN

[Viungo vyote vinaelekeza kwenye kurasa za intaneti za lugha ya Kihispania isipokuwa ikielezwa vinginevyo.]

Tetemeko  kubwa lenye vipimo vya tetemeko 8.3 limeitikisa sehemu ya kaskazini mwa Chile na Kusini mwa Peru, pamoja na maeneo ya jirani nchini Bolivia, saa za jioni siku ya Jumanne ya April mosi, 2014, hali iliyosababisha tishio la tsunami kwenye ukanda huo wa pwani.

Watu sita wameripotiwa kupoteza maisha nchini Chile, ikiwa ni pamoja na mwanamme mmoja raia wa Peru. Nchini Peru, hakuna taarifa za madhara makubwa katika majiji matatu ambapo nguvu ya tetemeko hilo ilikuwa kubwa zaidi – Tacna, Moquegua na Arequipa.

Raia wa Peru waliingia kwenye mtandao wa Twita wakati na baada ya tetemeko hilo. Ilisemekana kuwa kwenye jiji la Tacna hapakuwa na umeme kufuatia kuangua kwa nguzo za umeme:

Kwenye jiji la Tacna, mtikisiko ulikuwa mkubwa, jiji halina umeme.

Taarifa kutoka kwenye kituo cha Radio cha La Linterna kilitoa taarifa za kina zaidi:

Taarifa kutoka Tacna zinasema kuna tetemeko kubwa limetokea huko sekunde kadhaa zilizopita.

Kwa mujibu wa taarifa zilizokuwa zinatangazwa, hapakuwa na umeme wala huduma ya mawasiliano ya simu za mkononi mjini Moquegua:

Maeneo ya Tacna na Moquegua hayana umeme. huduma za makampuni ya simu ya Movistar na Claro hazipatikani baada ya tetemeko…

Kutoka Chile zilikuja ripoti za watu kutakiwa kuhama makazi kwenye maeneo ya ukanda wa pwani ya kaskazini kuchukua tahadhari dhidi ya uwezekano wa tsunami:

HABARI MPYA – Zoezi la kuwahamisha watu kaskazini mwa Chile lilifanyika kwa utulivu, kwa mujibu wa mwandishi wetu aliyeko Arica.

PICHA: Hivi ndivyo sehemu za pwani ya Chile zinavyohamwa kufuatia tishio la tsunami.

Hali kadhalika, kulikuwa na amri ya kuhama makazi nchini Peru  baadhi ya majiji kusini mwa nchi hiyo:

DHARURA: Amri ya kuhama makazi kwenye pwani ya Peru: Arequipa, Ica, Tacna.

DHARURA – TETEMEKO NCHINI CHILE: Mamlaka za Peru zimeliambia shirika la habari la AFP kuwa zinawahamisha watu kwenye eneo la kusini la nchi hiyo.

DHARURA – TETEMEKO NCHINI CHILE: Njia zote kuelekea [pwani ya Lima] Costa Verde kutoka [wilaya za] San Miguel, Magdalena, San Isidro, Miraflores na Barranco jijini Lima.

Mawimbi ya kwanza ya tsunami yaliripotiwa kuonekana kwenye pwani za Ilo na Tacna kusini ya Peru:

Mawimbi ya Tsunami yaliwasili La Punta Callao saa 2:31 jioni., Ica saa 1:39, Tacna na kwa mji wa Moquegua hayo ndiyo yanawasili.

Wakati huo huo nchini Chile, kuna taarifa za mitikisiko midogo baada ya tetemeko:

CHILE: Mitikisiko isiyopungua mitano ilitokea baada ya tetemeko hilo kubwa. Hizi ni nchi zenye hatari ya kukubwa na tsunami.

1 maoni

  • Kiungo cha makala haya kutokea kwenye tovuti nyingine: Tetemeko Kubwa Lizitikisa Chile na Peru | TravelSquare

    […] Tetemeko Kubwa Lizitikisa Chile na Peru Picha imechukuliwa kutoka kwa mtumiaji wa Twita @24HorasTVN [Viungo vyote vinaelekeza kwenye kurasa za intaneti za lugha ya Kihispania isipokuwa ikielezwa vinginevyo.] Tetemeko  kubwa lenye vipimo vya tetemeko 8.3 limeitikisa sehemu ya kaskazini mwa Chile na Kusini mwa Peru, pamoja na maeneo ya jirani nchini Bolivia, saa za jioni siku ya Jumanne ya April mosi, 2014, hali iliyosababisha tishio la tsunami kwenye ukanda huo wa pwani. Watu sita wameripotiwa kupoteza maisha nchini Chile, ikiwa ni pamoja na mwanamme mmoja raia wa Peru. Nchini Peru, hakuna taarifa za madhara makubwa katika majiji matatu ambapo nguvu ya tetemeko hilo ilikuwa kubwa zaidi – Tacna, Moquegua na Arequipa. Raia wa Peru waliingia kwenye mtandao wa Twita wakati na baada ya tetemeko hilo. Ilisemekana kuwa kwenye jiji la Tacna hapakuwa na umeme kufuatia kuangua kwa nguzo za umeme: En la ciudad de #Tacna se sintió fuerte el movimiento, la ciudad esta sin energía eléctrica #AlertaNoticias — Danitza Lawless (@danitza_pf) April 2, 2014 Kwenye jiji la Tacna, mtikisiko ulikuwa mkubwa, jiji halina umeme. Taarifa kutoka kwenye kituo cha Radio cha La Linterna kilitoa taarifa za kina zaidi: Reporte desde #Tacna a raíz del fuerte sismo que se ha sentido hace instantes https://t.co/WsgiyWVooG — La Linterna Radio (@LalinternaP) April 2, 2014 Taarifa kutok… Kusoma makala kamili  »  http://sw.globalvoicesonline.org/2014/04/tetemeko-kubwa-lizitikisa-chile-na-peru/ […]

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.