Zimbabwe: Robert Mugabe Ashinda Uchaguzi, Atuhumiwa Kuiba Kura

Rais Robert Mugabe ameshinda uchaguzi wa Rais nchini Zimbabwe ulifanyika Jumamosi ya Julai 31, 2013, akimbwaga mshindani wake wa karibu, waziri mkuu wa zamani katika serikali ya umoja wa kitaifa Morgan Tsvangirai.

Uchaguzi huo umekuwa wa amani kwa mara ya kwanza tangu kuanzishw akwa serikali ya pamoja kati ya chama cha Zanu PF cha Mugabe na chama kikuu cha upinzani kinachoongozwa na Tsvangirai kiitwacho Movement for Democratic Change (MDC). Serikali ya pamoja ilianzishwa kufuatia uchaguzi uliopita wa mwaka 2008 ulisemekana kuvurugwa mno na kusababisha umwagaji wa damu.

Mugabe, mwenye umri wa miaka 89 na ambaye amekuwa madarakani kwa miaka 33, ataendelea kuitawala nchi hiyo kwa miaka mingine mitano. Waangalizi wa uchaguzi huo kutoka Umoja wa Afrika (AU) na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Afrika ya Kusini (SADC) wameunga mkono uchaguzi wa Mugabe pamoja na madai ya udanganyifu mkubwa yanayotolewa na upinzani.

Botswana, hata hivyo, ni nchi pekee ya Afrika iliyotoa wito wa ukaguzi huru wa uchaguzi huo. Baadhi ya wnaachama wa SADC wamethibitisha kuyaunga mkono matokeo hayo kwa kudai kuwa uchaguzi ulikuwa huru “lakini si lazima uwe wa haki.”

President Robert Mugabe is the second oldest presidential candidate in Africa. Photo released to the public domain by the U.S. federal government.

Rais Robert Mugabe ni mtawala mzee kuliko wote barani Afrika. Picha imeruhusiwa kutumiwa na umma na serikali ya Marekani.

Uchaguzi ulifanyika pamoja na maandamano kutoka kwa washirika wa muungano wa Mugabe na raia wa Zimbabwe baada ya *Mugabe) kujitangazia mwenyewe kuwa Julai 31, 2013 ndiyo tarehe ya uchaguzi. Mahakama ya Katiba ilimwamuru Robert Mugabe kuitisha uchaguzi tarehe 31 Julai kufuatia kufanikiwa kwa maombi ya Jealousy Mawarire, mkurugenzi wa Kituo cha Uchaguzi na Demokrasia kwa eneo la Afrika ya Kusini (CEDSA).

Kwa kutumia alama habari #ZimElections, #ZimbabweDecides, #ZimDecides na #ZimbabweElections, watumiaji wa Twita kutoka sehemu mbalimbali za dunia walitoa maoni yao kuhusiana na ushindi wa Mugabe.

Mzambia anayeishi Uingereza na mwanzilishi wa CrossFire Radio, Mueti Moomba (@Muweight) alishangaa nani alimpigia kura mtawala huyo mzee wa miaka 89:

Mjasiria mali wa kijamii wa Zimbabwe Sir Nigel (@SirNige) hakukata tamaa:

Andiva (@AndyAndiva) kutoka Kenya anakilaumu chama cha upinzani cha MDC kwa kushiriki uchaguzi uliovurugwa:

mwandishi wa Afrika Kusini na mshauri wa matangazo Thebe Ikafaleng (@ThebeIkafaleng) alimnukuu Tendai Biti, Katibu Mkuu wa MDC, aliwakejeli wale waliokuwa wakihoji uwepo wa watu milioni mbili waliokwisha kufa katika daftari la wapiga kura haukuathiri upinzani:

Uchaguzi wa Zimbabwe (@ZimElections) umeonyesha ukubwa wa tatizo la wapiga kura mfu:

rakim allah (@LDaviano) alitoa maoni kwenye suala hilo hilo la “wapiga kura wafu”:

Azad Essa wa Al Jazeera(@azadessa) alihoji tathmini ya Umoja wa Afrika kwa uchaguzi huo:

Mwandishi wa Habari za Uchunguzi na Mtengenezaji wa filamu Stanley Kwenda (@stanleykwanda) alibainisha kuwa ushiriki wa polisi inawezekana uliwatisha wapiga kura wasio na uelewa:

mfanya biashara wa Afrika Kusini Another_craig (@@Another_craig) alitwiti kuhusu taarifa ya mwanajeshi mwenye miaka 135 “aliyepiga kura” katika uchaguzi huo:

Akimjibu @Another_craig, mjasiria mali wa Afrika Kusini Sello Rabele (@sellorabs) alindaika kwamba anatamani kuwa mwanajeshi akikua:

arnold chamunogwa (@chamunogwa) hakuonyesha kushangaa kuwa chama tawala kimeiba kura. Alishangazwa na suala jingine kabisa:

Akuzike Polela (@Mulengi) kutoka Zambia alibainisha kwamba Morgan Tsvangirai ana rafiki mmoja wa ki-Afrika:

Zimbabwean Kudzai (@shuestrait) ningependa kuwaona wa-Zimbabwe wanaoishi nchini humo wakiamua kile kilicho chema kwa ajili ya nchi yao:

Mkenya David Ogara (@david_ogara) alifanya hitimisho chungu kuhusu uchaguzi wa Afrika:

1 maoni

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.