Peru: Mchezaji wa Kandanda Afariki Dunia Uwanjani

Dakika tano kabla ya kumalizika kwa mchezo kati ya timu zaReal Garcilaso na Sporting Cristal, mchezaji nyota wa timu ya Sporting Cristal mwenye miaka 18 Yair José Clavijo alipata mshituko wa moyo na akapoteza maisha. Madaktari wa timu hiyo walijaribu bila mafanikio kunusuru hali yake akiwa kwenye sehemu ya kuchezea katika uwanja wa Manispaa ya Urcos, katika mkoa Cusco.

Mtangazaji wa zamani wa kandanda Elejalder Godos [es] aliungana na watumiaji wa mtandao wa Twita ambao waliamua [es] kuingia kwenye mtandao huo kuonyesha hisia zao kuhusu habari hizo za kusikitisha:

Rambirambi zangu kwa familia ya Yair Clavijo kwa kifo cha ghafla cha mchezaji kinda wa timu ya Sporting Crital akiwa uwanjani.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.