Maelfu ya Wafanyakazi Waandamana Barani Asia

Global Voices inayapitia kwa haraka maandamano ya Siku ya Wafanyakazi Mei Mosi kwenye nchi za Cambodia, Filipino, Indonesia na Singapore. Mikutano, ambayo iliandaliwa kudai haki za wafanyakazi na makundi mengine ya utetezi, yalifanyika kwa amani katika bara lote la Asia ya Kusini Mshariki.

Nchini Cambodia, zaidi ya wafanyakazi 6,000 wa kiwanda cha nguo waliungwa mkono na wanafunzi, Mashirika yasiyo ya Kiserikali, na wakazi masikini wa mijini katika Jiji la Phnom Penh ambao wote kwa pamoja waliandamana kutokea Viwanja vya Freedom Park kuelekea kwenye Bunge la nchi hiyo kutoa wito wa kuboreshewa maslahi yao pamoja na mazingira bora zaidi ya kazi.

Garment workers march in Phnom Penh, Cambodia. Photo from Licadho

Wafanyakazi wakiandamana jijini Phnom Penh, Cambodia. Picha Licadho

Cambodian protesters near the National Assembly

Waandamanaji wa Cambodia karibu na Bunge la Nchi hiyo. Picha na Licadho

Katika video hii iliyowekwa na Kituo cha Jamii cha Elimu ya Sheria, muhutasari wa madai makubwa na hali ya wafanyakazi wa Cambodia ulikuwa:

Nchini Indonesia, maelfu ya wafanyakazi waliandamana mbele ya Ikulu ya nchi hiyo jijini Jarkata kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi. Baadhi ya madai yao, yalikuwa “kuongezwa kwa kima cha chini cha mshahara, bima ya afya na usalama kwa wafanyakazi, pamoja na kukataa misaada ya nje.”

Thousands of workers march in Jakarta. Photo by Ibnu Mardhani, Copyright @Demotix (5/1/2013)

Maelfu ya wafanyakazi wakiandamana jijini Jarkata. Picha na Ibnu Mardhani, Kwa idhini ya @Demotix (5/1/2013)

Workers march in Jakarta during Labor Day. Photo by Ibnu Mardhani, Copyright @Demotix (5/1/2013)

Wafanyakazi wakiandamana jijini Jarkata siku ya Mei Mosi. Picha na Ibnu Mardhani, Kwa idhini ya @Demotix (5/1/2013)

Nchini Ufilipino, kikundi cha wafanyakazi kiitwacho Kilusang Mayo Uno kilikatishwa tamaa na sera za kazi zinazotekelezwa na serikali:

TUnaadhimisha mwaka wa 127 wa Siku ya Wafanyakazi Kimataifa na mwaka 110 wa maadhimisho hayo nchini Ufilipino kwa maandamano ya kitaifa kupinga utawala usiojali maslahi ya mfanayakazi na unaoshabikia ubepari wa Rais Noynoy Aquino.

Aquino ameyakataa madai ya wafanyakazi ya kupandisha mishahara yao, kuachana na mfumo wa ajira za mkataba na kusimamishwa kwa ukandamizaji unaofanywa na vyama vya wafanyakazi. Amejitetea kwa kutengeneza mfumo wa kuwanufaisha wafanyakazi pamoja na juhudi za serikali kuzalisha ajira.

Filipino workers march near the presidential palace demanding higher wages and rollback of prices. Photo from Facebook of Tine Sabillo

Wanafanyakazi wa ki-Filipino wakiandamana karibu na Ikulu ya Rais wakidai kupandishiwa mshahara na kudhibiti mfumuko wa bei. Picha kutoka kwenye ukurasa wa facebook wa Tine Sabillo

Labor Day rally in the Philippines. Photo from Facebook of Tine Sabillo

Mkutano wa Mei Mosi nchini Ufilipino. Picha kutoka kwenye ukurasa wa Facebook wa Tine Sabillo

Dondoo za matukio ya Mei Mosi jijini Manila zilikusanywa katika video hii iliyowekwa mtandaoni na EJ Mijares:

Nchini Singapore. Gilbert Goh wa tovuti ya transitioning,org aliandika kuhusu maandamano hayo ya kihistoria ya wafanyakazi nchini Singapore:

Tumejua kuwa nasi pia tunatengeneza sehemu nyingine ya historia nchini Singapore kwa kuwa haikuwa kutokea mtu akahamasisha tukio la siku ya wafanyakazi kutokea chini kabisa -haijawahi kutokea na tunajisikia fahari kufanya hivyo kwa mara ya kwanza!

Kwa sasa tunaweza hata kupanga kufanya maandamano ya wafanyakazi wakati wa Mei Mosi kuanzia sasa -kama inavyofanyika katika nchi nyinginezo kwa miongo sasa.

Thousands of Singaporeans assembled in Hong Lim Park on Labor Day. Photo from Facebook of Lawrence Chong

Maelfu ya wa-Singapore wakiwa wamekusanyika katika Viwanja vya Hong Lim Mei Mosi. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa Lawrence Chong

Singaporeans participate in historic Labor Day protest to air their views on the government's population policy paper. Photo from Facebook of Lawrence Chong

Wa- Singapore wakishiriki katika Maandamano ya kihistoria ya Wafanyakazi kufikisha kilio chao kwa serikali kuhusu andiko lake la sera ya idadi ya watu. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa Lawrence Chongg

Tukio hili ni kupinga tukio la mwezi Februari lililowakusanya maelfu ya wa-Singapore waliokuwa wanapinga pendekezo la serikali kuhusu sera ya mpya ya idadi ya watu. Katika video hii, wa-Singapore wanaeleza sababu zao za kuandaaa na kuunga mkono tukio hilo.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.