Ufilipino: Mafuriko Yaathiri Vitongoji vya Jiji la Manila na Mikoa ya Karibu

 

Mvua kubwa imesababisha mafuriko makubwa katika maeneo mengi ya Vitongoji vya jiji la Manila na mikoa ya jirani katika Kisiwa cha Luzon nchini Ufilipino. Eneo la katikati ya Manila, ambalo ndipo penye shughuli nyingi zaidi za mjini katika nchi hiyo hasa kwa kuwa linaundwa na miji 17 pamoja na manispaa mbalimbali, limeathiriwa vibaya. Tayari serikali imesitisha shughuli za shule, kazi katika ofisi za uma na hata zile za binafsi.

 

Picha zilizo hapa chini, zinazotoka hasa kwenye kurasa za Facebook na Twita, zinaonyesha kiwango cha mafuriko katika maeneo ya jiji na huenda hali itakuwa mbaya zaidi kwa sababu bado mvua inaendelea kunyesha hadi tunapoandika makala haya.

 

Strong rain in Metro Manila and nine other provinces. Photo from Philippine government Facebook page.

Mvua kubwa katika vitongoji vya Manila na majimbo mengine tisa. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa serikali ya Ufilipino

Another map showing the areas affected by rains and floods. Photo from Facebook page of Nadja De Vera.

Ramani nyingine ikionyesha maeneo yalioathiriwa na mvua na mafuriko. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa Nadja De Vera

Dark clouds hover above downtown Manila. Photo from Facebook page of Lorrelyn Ocampo.

Mawingu meusi yaliyotanda katikati ya jiji la Manila. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa Lorrelyn Ocampo.

Flood in Asia's oldest Catholic university. Photo from Facebook page of Dexter Aquitania Austria.

Mafuriko katika chuo kikuu kikongwe zaidi cha Kikatoliki barani Asia. Picha kutoka ukurasa wa Faceebook wa Dexter Aquitania Austria.

Photo of flooding in Marikina, showing street lights. Photo from Facebook page of Chris Velasco.

Picha ya mafuriko katika mji wa Marikina, ikionyesha taa za barabarani. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa Chris Velasco.

River overflowing in Montalban, Rizal located east of Manila. Photo from Facebook page of Maria Fema Duterte.

Mto uliofurika huko Montalban, Rizal mashariki ya Manila. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa Maria Fema Duterte.

Flood in Morayta near the country's university zone. Photo from Facebook page of AiRon Sulit.

Mafuriko huko Morayta karibu na chuo kikuu cha Serikali ya eneo hilo. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa AiRon Sulit.

Flooding in San Juan City. Photo from Twitter page of @michelleorosa.

Mafuriko katika Mji wa San Juan. Picha kutoka ukurasa wa Twita wa @michelleorosa

.Mafuriko katika barabara ya chini ya Ayala katika eneo lenye shughuli nyingi nchini humo. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa Joel Garzota Vmobile.

 Mafuriko katika Barabara ya chini ya Ayala iliyo katika eneo lenye shughuli nyingi sana nchini humo. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa Joel Garzota Vmobile.
Flood in Bacoor, Cavite located south of Manila. Photo from Facebook page of ASAP XV.

Mafuriko huko Bacoor, Cavite kusini mwa Manila. Picha kutoka ukurasa wa Facebook wa ASAP XV.

Flood in Bocaue, Bulacan located north of Manila. Photo from Facebook page of Almond Andres.

Mafuriko huko Bocaue, Bulacan kaskazini mwa Manila. Picha kutoka ukurasa wa facebook wa Almond Andres.

 

Serikali imetoa orodha ya maeneo yaliyokumbwa na mafuriko katika Vitongoji vya jiji la Manila. Orodha nyingine inaonyesha barabara ambazo bado zina mafuriko mengi. Mashirika ya habari pia yamekusanya orodha za vituo vya uokoaji na shughuli za uokoaji katika maeneo ya jiji.

 

Watumiaji wa mtandao wa Twita wanatumia alama ashiria #rescueph na #prayforthephilippines kufuatilia hali hiyo. Hapa chini kuna twiti ya kuwakumbusha waandishi wa habariambao wanaoripoti maafa yanayojitokeza:

 

@katray: Marafiki wa vyombo vya habari, tunathamini kazi mnayofanya. Ningetamani waandishi wa habari wawe wasioathiriwa na maji, lakini sivyo ilivyo, ninawatakia heri na salama. Jitunzeni Marafiki ;)

Carl Ramota anaonyesha kufedheheshwa na kuchelewa kwa serikali kuchukua hatua, hasa Rais:

Mpendwa serikali ya Aquino, ilikupasa kufanya mkutano na vyombo vya habari jana usiku au mapema leo asubuhi. Hatutaki kukuona wewe umevaa vazi la kuzuia mvua au koti katika chumba cha mkutano, ukizungumza juu ya mambo ambayo sisi tayari tunayajua au sasa yanaendelea. Panda vyombo vya majini na uzungukie ili kukagua maeneo yote yaliyoathiriwa na mafuriko. Nenda katika vituo vya uokoaji na saidia kusambaza misaada. Fanya kitu! Sio kukaa tu huko na kuzungumza! Vichwa havina budi kufanya kazi.

Carlo Ople anabainisha wajibu wa vyombo vya habari vya kisasa katika kueneza taarifa kuhusu mafuriko:

 

Haraka kama mafuriko yalivyoenea watu walianza kuchukua picha na kuziweka kwenye mitandao ya Facebook na Twita. Mtandao mmoja ulianza kushirikiana na mtandao mwingine, na kubadilishana huku kwa taarifa kuliendelea hadi picha hizo zikaenea sana. Kupitia picha hizo ilikuwa rahisi kuona jinsi hali halisi ilivyokuwa mbaya.

1 maoni

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.