Habari kutoka 24 Machi 2012
Palestina: Gaza yashambuliwa, watu 12 wauwawa na wengine wengi kujeruhiwa
Usiku kucha wa tarehe 9 Machi na asubuhi ya Machi 10, ndege za kivita za Israel zilishambulia maeneo maalumu katika Ukanda wa Gaza, na kuua takribani watu 12 na kujeruhi wengine 20.
Iran: Wachora katuni ‘wamkalia kooni’ Khatami kwa kupiga kura
Mohammad Khatami, aliyekuwa Rais mwanamageuzi wa Irani, Ijumaa ya tarehe 2 Machi, 2012 alipiga kura katika uchaguzi wa wabunge. Kitendo hicho kilikinzana na kauli aliyopata kutoa siku za nyuma kwamba angegomea kupiga kura hadi wafungwa wote wa kisiasa waachiwe huru na katiba kuheshimiwa. Kitendo chake hicho kimezua shutuma nyingi kutoka kwa wanamageuzi walio makini katika kugomea uchaguzi huo.
Amerika Kusini: Waathirika wa ‘biashara’ ya kukuza matiti waingia mtandaoni
Wanawake wengi wameungana kwenye tovuti za kijamii kusema wanachofikiri na kubadilishana taarifa kuhusu matatizo yanayosababishwa na viini vya kukuzia matiti. Wakati huohuo wanapanga hatua gani za kisheria wachukue. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ugonjwa wa saratani huko Amerika ya Kusini. Je, ni kina nani hawa wanaopaaza sauti zao barani humo? Fuatilia ...