Februari, 2011

Habari kutoka Februari, 2011

Gabon: Wanafunzi Waandamana, Wanajeshi Wasambazwa

Mgogoro wa kisiasa nchini Gabon ulifikia vilele vipya siku ya Alhamisi, wakati wanafunzi walipoandamana katika Chuo Kikuuu cha Omar Bongo kilichopo ndani ya mji mkuu wa nchi hiyo, Libreville. Wakati maandamano ya juma lililopita yalishirikisha zaidi wanachama wa vyama vya upinzani, mgogoro huu unaonekana kupelekea kuwa mgogoro mkubwa zaidi wa kijamii.

Misri: Picha Zinapoongea Zaidi Ya Maneno

Kadri ya watu milioni tayari wapo kwenye viwanja vya (Ukombozi) vya Tahrir jijini Cairo wakiimba, na kumtaka Mubarak aondoke. Maandamano ya kumpinga Mubarak yamekuwa yakifanywa nchini misri kwa siku 11 mfululizo na siku ya leo imepewa jina la Ijumaa ya Kuondoka au Ijumaa ya Mwisho. Hapa kuna baadhi ya picha zilizotumwa kwa njia ya Twita na watu waliopo kwenye eneo hilo, zinazoonyesha umma unaoandamana kuelekea kwenye viwanja (vya Tahrir), wanavyopekuliwa kwa makini katika vituo vya ukaguzi vilivyowekwa ili kuwalinda waandamanaji wa amani mbali na wahuni waliolipwa na serikali.