Septemba, 2008

Habari kutoka Septemba, 2008

Sheria inapokwaza haki za binadamu …

  29 Septemba 2008

Mtoto mwenye umri wa shule ya msingi aliyepatikana nje ya ndoa huko Zhuhai, kusini mwa China, hakubaliwi kujiunga na shule, kwa sababu mama yake hawezi kulipa faini kubwa ya kuwa na "mwana haramu", habari hii inasimuliwa na bloga, Han Tao.

Angola: Uchaguzi Katika Picha

  22 Septemba 2008

Waangola wako katika uchaguzi kwa mara ya kwanza katika miaka 16 - uchaguzi bado unaendelea Jumamosi hii katika vituo 320 jijini Luanda. Mpaka sasa, hakuna matukio yoyote yaliyoripotiwa, na moyo wa utu umedumu, kama ilivyoangaliwa na mpiga picha Jose Manuel da Silva.

Msumbiji: Mgogoro wa Kisiasa Katika Jimbo la Kati la Beira

Waunga mkono wa Renamo wenye hasira walimwagika katika mitaa ya Beira ili kupinga uamuzi wa chama wa kumbadilisha Meya aliyeko madarakani Bwana Davis Simango na kumuweka Manuel Pereira kama mgombea wa kiti cha serikali ya manispaa katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Mwezi Novemba 2009. Mwanahistoria Egidio Vaz anaandika barua ya wazi kwa Rais wa Renamo, Bwana Alphonso Dhlakama katika blogu yake.

Irani: Redio Zamaneh, Redio ya Mabloga

  21 Septemba 2008

Redio Zamaneh ni redio ya lugha ya kipersia yenye makao yake huko mjini Amsterdam. Zamaneh ni neno linalomaanisha “wakati” katika lugha hiyo. Redio Zamaneh (RZ) ni chombo huru cha utangazaji kilichosajiliwa kama asasi isiyo ya kiserikali huko Uholanzi, kikiwa na studio na makao yake makuu mjini Amsterdam. Mratibu wa redio...

Colombia: Watu Wanaswa na Mitego ya Upatu

  14 Septemba 2008

Kwa kupitia picha za video na mtandao wa marafiki wa Facebook, raia wa Colombia, Diego Alejandro, anaweka wazi udanganyifu na utapeli mkubwa uliojificha nyuma ya michezo ya upatu ambayo inatangazwa kama njia mbadala za uwekezaji. Katika nchi ambapo akaunti za benki zimepoteza maana kwa sababu ada za uendeshaji ziko juu kuliko riba anayopata mwenye akaunti, michezo hii ya upatu inayoshawishi kumjaza mtu mapesa, ambapo raia wanalipa kiasi fulani cha pesa ili kujiunga na kisha kuingiza marafiki zao 7 kabla wao hawajaanza kufurahia riba ya juu ajabu (kati ya asilimia 40 mpaka 70) basi imekuwa ni kivutio kikubwa mno.

Jordan: Ubloga wa Video wa Malkia Rania

  12 Septemba 2008

Chombo cha habari cha Blogger Times kinachoendeshwa na mabloga wa Kiarabu, kimemtaja Malkia Rania wa Jordan kuwa bloga maarufu zaidi wa video za kutoka Uarabuni katika chombo cha Video mtandaoni, YouTube, kufuatia mafanikio ya mlolongo wa video za YouTube aliouanzisha kuondoa dhana potofu dhidi ya Waarabu.

Paraguai: Rais Lugo Kutopokea Mshahara

  12 Septemba 2008

Utawala wa Rais Ferdinand Lugo umeanza na tangazo kuwa hatapokea mshahara wake wa mwezi. "Sihitaji mshahara huo, ambao unapaswa kumilikiwa na masikini," alisema Lugo. Mabloga nchini humo wanatofautiana mitazamo, wakati mmoja anausifu uamuzi huo, mwingine anajiuliza ni vipi Rais lugo atajilipia gharama binafsi za maisha.

Paraguai: Kuapishwa Kwa Lugo Kwenye Flickr

  12 Septemba 2008

Rais wa paraguai alianza kutumia Flickr mnamo januari 2008 kama njia ya kuorodhesha nyendo zake wakati wa kampeni. Baada ya kuapishwa kama rais wa nchi siku ya tarehe 15 Agosti, anaendelea kutumia chombo hiki cha uandishi wa kijamii. Karibia picha 2,500 baadaye na zote chini ya haki miliki huria, Lugo anategemea kuwajumuisha WaParaguai nyumbani na ughaibuni katika urais wake.

Nia ya Mwanablogu Mmoja Kumsaidia Mtoto Kamba huko Madagaska

Sauti Chipukizi  6 Septemba 2008

Ikiwa unataka kwenda sambamba na habari mpya mpya kutoka Madagaska, inawezekana kabisa ukawa ni msomaji wa Madagascar Tribune. Na kama wewe ni mdau wa gazeti hilo, hivi karibuni yawezekana ulishakutana na habari iliyoandikwa na mwandishi wa habari Herimanda R kuhusu upasuaji wa maradhi ya nadra na mafanikio yake ambao ulifanyika...